Katika jitihada za Serikali kuwezesha wananchi kiuchumi na kuongeza ajira kwa vijana, wanawake na makundi ya mahitaji maalumu, Serikali ya awamu ya sita katika moja ya vipaumbele vyake, imeanzisha kongani za Viwanda. Hii ni katika kuhamasisha uanzishwaji wa viwanda vidogo na vya kati na kuongeza ajira.
Katika kutekeleza hayo, Meneja wa SIDO Mkoa wa Mtwara alikutana na Katibu Tawala wa Mkoa, Bi Bahati Geuzye, ili kujadili namna ya kupata maeneo ya kongani za viwanda katika kila Wilaya ambapo wajasiriamali wataozalisha bidhaa mbalimbali watawekwa pamoja. Hii itarahisisha katika utoaji wa huduma mbalimbali za kuboresha uzalishaji, utengenezaji wa bidhaa bora, na uongezaji ajira zaidi kwa vijana na wananchi wa Mkoa wa Mtwara

