KAMISHNA WA JESHI LA MAGEREZA TANZANIA ATEMBELEA BANDA LA SIDO
Imewekwa: 03 Jul, 2026
KAMISHNA WA JESHI LA MAGEREZA TANZANIA ATEMBELEA BANDA LA SIDO

Kamishna wa Huduma za Urekebu ndani ya Jeshi la Magereza Tanzania na Uwezeshaji Kiuchumi, Bi. Amina Jumanne Kavirondo, alitembelea Banda la SIDO katika Maonesho ya 50 ya Kimataifa ya Biashara ya Dar es Salaam (DITF), 2026  ambapo alipata fursa ya kujionea bidhaa mbalimbali zinazozalishwa na Vituo vya kuendeleza Teknolojia za SIDO pamoja na bidhaa mbalimbali  zinatotengezwa na wajasiriamali  wanaonufaika na huduma za SIDO.

Katika ziara hiyo, alipewa maelezo kuhusu huduma mbalimbali zinazotolewa na SIDO katika kukuza ujasiriamali, kuendeleza viwanda vidogo na vya kati, pamoja na kuhamasisha uongezaji thamani wa mazao na bidhaa za ndani ili kuongeza ushindani wa bidhaa za Tanzania katika soko la ndani na nje ya nchi.

Alizungumzia kuhusu kuzidisha mashirikiano  hasa katika  kuwawezesha wafungwa kiuchumi ili pindi wanavyomaliza kutumikia vifungo vyao waweze pia kuendelea na ujuzi ambao watakuwa wameupata wa kutengeneza vitu mbalimbali.

Matangazo
03 Dec, 2025
23 Nov, 2025
Feedbacks

Mrejesho, Malalamiko au Wazo