Karibu

Ninayo furaha kuwakaribisha kutembelea  tovuti ya Shirika la Maendeleo ya Viwanda  Vidogo (SIDO). SIDO ni muhimili muhimu wa Serikali katika kukuza na kuendeleza viwanda vidogo na vya kati nchini  kwa lengo la kuchochea maendeleo ya uchumi wa Taifa na ustawi wa wananchi.

Huduma zinazotolewa na Shirika zinawawezesha wajasiriamali kujenga uwezo wao wa kuzalisha na kufungasha bidhaa zenye kukidhi viwango vya soko. Huduma hizo ni mafunzo na ushauri wa kibiashara; utengenezaji wa teknolojia zinazozalisha na kuchakata malighafi aina tofauti; masoko na uwekezaji; pamoja na huduma za mikopo.

Tovuti yetu ya www.sido.go.tz itakupa taarifa mbalimbali  kuhusu ratiba za mafunzo  na maonesho; matukio ya kijasiriamali;  na mafanikio kutoka kwa baadhi ya wajasiriamali. Pia, tembelea katika kurasa zetu za mitandao ya kijamii (sidotanzania) ili kuendelea kupata taarifa muhimu zitakazoendelea kukupa uelewa wa Shirika letu.


Karibuni sana!

 

Mhandisi Profesa Sylvester Mpanduji

Mkurugenzi Mkuu - SIDO

Matangazo
03 Dec, 2025
23 Nov, 2025
Feedbacks

Mrejesho, Malalamiko au Wazo